Kilio cha Familia Bungoma

Famili moja kutoka eneo la Ndengelwa kaunti ya Bungoma sasa imeitaka serikali ya Kenya na ile Canada kuingilia kati na kuwasaidia ili wakaweze kusafirisha mwili wa mpendwa wao na kumzika nyumbani kwao katika kijiji cha Ndengelwa.Elizabeth Nekesa ambaye ni  mamake marehemu anadai  kuwa Leonard Wandili aliyesafiri nchini Canada kikazi alifariki akiwa huko huku familia yake ikikosa kujua kiini cha kifo cha mpendwa wao .“Niliachana na mtoto wangu tarehe mbili akiwa mzima, naomba mwili ufanyiwe upasuaji ili nielezwe mwanangu alikufa kivipi,mtoto alienda huko kikazi ,wanisaidie mwili wa mtoto wangu urudi kenya”…Kwa sasa familia hiyo imeitaka serikali hizi mbili kuwasaidia ili wakaweze kujua kiini cha kifo cha mpendwa wao na mwili wake kusafirishwa nchini Kenya ili akaweze kuzikwa na familia yake kulingana na desturi na mila za jamii ya Bukusu.

2356 232

Suggested Podcasts

Chris Hoff PhD(c), LMFT

The Latin American Fashion Summit

Rana Campbell

Marty Called

Louis Polak

Abbas Riza

Ajith Jojo