SE7EP14 - SALAMA NA COACH EVARIST | FIRST QUARTER

Evarist Mapunda ni moja wa makocha wangu wa maisha haya ninayoishi sasa hivi, ananifahamu toka nikiwa na miaka 17 mpaka sasa hivi ingawa hapa katikati baada ya ‘kuwa mkubwa’ nilipoteana nae kwenye mahangaiko ya kujitafuta na kutafuta maisha. Ila Mimi na yeye tunajua kila mmoja wetu ni mtu wa aina gani na anamaanisha NINI kwa mwengine.

Ukiwauliza watoto na wakubwa wengi wa Upanga watakuambia nini yeye pia anamaanisha kwenye maisha yao, lazima atakua na simulizi kuhusu mwalimu huyu hodari wa basketball na maisha, kama hadithi hiyo itakua haimhusu yeye directly badi itakua inamhusu Ndugu yake au mtoto wake au hata rafiki yake, na kama itakua hana hao wote basi hata ya kusikia atakua nayo.

Coach Evarist ni mmoja ya watu ambao wamesaidia kwa kiasi kikubwa mno vijana wa miaka ya 2000 kuwa na HESHIMA ya maisha, Heshima ya kazi na miili yao, kama umepita kwenye mikono yake basi utakua unajua hilo. Na kama ule usemi wa Kiswahili unaosema ‘majuto ni mjukuu’ basi ndo faida za yale alotufundisha sisi tunayaona. Tunayaona baada ya kukua maana wakati anatufundisha heshima ya muda na drills ngumu za basketball tulikua tunaona anatuonea sana sana. Binafsi nilikua naona hivyo, nilikua naona kama hanipendi maana kila mara yuko kwenye shingo yangu kuniambia lipi sijafanya vizuri. Sasa hivi nikikaa na kujiuliza kipi hasa kilinifanya nihame Pazi na kwenda kucheza basketball yangu Don Bosco ukiachana na kwamba rafiki zangu wengi walikua kule sasa ndo jibu linakuja kwamba Coach Evarist naye alichangia kwa kiasi kikubwa mimi kuamua hilo. Alikua kijana, mwenye kuujua mchezo na Don Bosco Queens ilikua ni moja ya team BORA zaidi za wasichana kuwahi kutokea miaka hiyo. Wengi wao nilikua aidha nimesoma nao Makongo au nimeenda nao Umiseta mara kadhaa kwahiyo maamuzi yangu hayakua ya kuwaza sana ingawa Pazi ndo ilikua nyumbani kwetu na itaendelea kuwa hivyo.

Coach Evarist pia ashawahi kukutana na mitihani kadhaa mikubwa katika maisha yake, ingawa wa yeye kupata ajali mbaya ya gari mwanzoni mwa miaka ya 2000 itaendelea kusimama kuwa mtihani mkubwa zaidi ambao amewahi kukabiliana nao, ukiachana na fainali tele ambazo yeye kama mchezaji au kocha ambazo zilikua dhidi ya timu ngumu na akawahi kushinda, huu ulikua wa aina tofauti sana. Alikua peke yake usiku wa manane wakati anaenda zake nyumbani baada ya kumaliza majukumu yake aliyojiongezea ya basketball ndo mtihani huo ulipomkuta, Coach Evarist anakumbuka idadi ya watu ambao walimzunguka na kumpiga vibaya baada ya ajali hiyo. Mungu pekee ndo anajua alimuokoa okoa vipi katika lile na kwenye operesheni zake zaidi ya kumi na tano ambazo amezifanya mpaka sasa hivi zinamfanya aishi na kwanini haya yote yametokea.

Coach Evarist ni muaminifu na mwingi wa imani, mpaka leo hii anaendelea kuishi maisha yake kama hakuna ambalo limemtokea na kubadilisha maisha na muonekano wake kwa maisha yake yote. Yule ambaye anakua na moyo kama ambao Coach Evarist anao pekee ndiye anayeweza kuishi kama ambavyo yeye anaishi. Ndo maana yeye ni wa kipekee sana.

Yangu matumaini maongezi yetu juu ya heshima na mustakabali wa mpira wetu wa kikapu na heshima juu ya mambo kadhaa yatakuvutia na kukufunza kitu. Yangu matumaini pia uta enjoy.

Love,

Salama.

--- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support

2356 232

Suggested Podcasts

Michael Stelzner, Social Media Examiner

Benjamin Light and Marco Sparks

Peter Labuza

MAHID (Mahla & Vahid)

WNYC Studios

The Grey Rooms Productions

True Story Tent

SHRI DEVKINANDAN THAKUR JI MAHARAJ

Beating hearts

DJ Infinizz (Prudhvi Reddi)